Showing posts with label Motivational speaker. Show all posts
Showing posts with label Motivational speaker. Show all posts

Tuesday, July 7, 2015

UMUHIMU WA ELIMU YA NAFSI NA UFAHAMU


Huwezi hata kidogo kutenganisha maisha ya mwanadamu na elimu ya saikolojia, elimu ambayo katika ulimwengu wa sasa wengi wanaisikia  lakini wachache wanaotambua umuhimu wake, achilia mbali maana ya neno lenyewe.  Mimi nimeona nikupe maarifa haya baada ya kuona mwenyewe inanisaidia na pia kupitia Asasi ya WEZESHA TRUST FUND imewasaidia wengi na watu wamepona magonjwa, wameshinda majaribu na leo hii wanafurahia kuifahamu naomba na wewe uwe mmoja wao ambaye ukisoma mada hii utajua jinsi ya kuenenda.

Injinia wa  kwanza aliyeipa nguvu elimu hiii ni  mwanasaikolojia  wa Kijerumani, Wilhelm Wundt ambaye alifungua maabara  na kutibu watu kwa kisaikolojia, zoezi ambalo  lilileta matokeo  ya kushangaza ulimwengu mzima.  Huo ulikuwa ni mwaka 1879.

Saikolojia ni ‘mtoto’ wa neno la Kigiriki lijulikanalo kama ‘psyche’ au akili na roho jina ambalo baadae  lilikuzwa  na kufahamika  kama ‘Psychology’, tafsiri  ikiwa Elimu ya Nafsi  na Ufahamu.  Katika nchi zilizoendelea somo hili linapewa nafasi  ya juu katika maisha ya binadamu kutokana na  umuhimu wake.  Wanasema wataalamu kuwa, kuishi  bila kujua tabia za vitu na watu pia na  ukuaji wake na kujifunza mabadiliko yake ni sawa na kutembea katika kamba ndogo ya maisha salama.  Unatakiwa ufahamu watu, wanyama, ndege na vitu vinavyokuzunguka ili uweze kushinda majaribu au changamoto zinazokuzunguka.

Saikolojia ni somo ambalo kila kukicha binadamu anatakiwa kufundishwa kwa vile hakuna anachoweza kukifanya kisiguse  akili na  nafsi  yake.   Inashauriwa  kwamba ni lazima mtu ajifahamu  mwenyewe pia awafahamu wengine, mazingira anayoishi na mabadiliko yake wakati wote, tunaishi katika nyakati na majira na unatakiwa ufahamu kila jambo linakupata linaanzia ndani yako mwenyewe.  Unaweza ukalitengeneza bila kufahamu au mazingira yakalitengeneza ukijua kabla haikusumbui.

Maswali ya msingi yenye kumuongoza  binadamu  vizuri katika  maisha yake ni  haya.  Mimi ni nani, kwa nini niko hivi?  Wale ni  watu ni akina nani?  Kwanini wako  vile na tunapaswa  kuwa vipi baadaye, pamoja na kujiuliza kwa nini vitu vipo kama vilivyo.
Imebainika kwamba, mvutano  wa nguvu za dunia na za binadamu huongezeka mara dufu kwa mtu ambaye hajui Saikolojia ya Maisha.   Dunia kama sayari na mwanadamu kama kiumbe kila  mmoja amekuwa akitengeneza  nguvu zake za kumuwezesha  kuwepo, huku uzalishaji  wa nguvu hizo kwa upande mmoja ukikinzana vikali na mwingine, hata hivyo madhara makubwa  yamekuwa yakiwakuta  binadamu ambao ndani yao kuna uhai ambao ni sisi wenyewe.

Hata hivyo, uchunguzi  unaonyesha kwamba ufahamu, nafsi na akili umebaki kuwa kinga muhimu ya mwanadamu katika  ulimwengu huu ambao umekuwa unabadilika  mara kwa mara.  Hatari iliyokuwepo siku hizi ni  hasa kwa ulimwengu huu wa tatu ni ukosefu wa elimu hii muhimu, jambao ambalo limewafanya watu  wenyewe kwa wenyewe kuzalishiana nguvu za kuangamizana  na kuiacha dunia  ikishinda mara zote na watu kupoteza maisha pasipo muda wao kufika au kuharibikiwa na mambo yao wakidhani ni hali ya kawaida.

Inahuzunisha  pia kufahamu  kwamba mbali  na binadamu kushindana na  mabadiliko  ya ulimwengu na nguvu zake, wengi wao  wamekuwa  wakipambana  na nguvu zao wenyewe ndani ya  miili yao bila kujijua, kiasi cha kupoteza maisha.

Tafiti za wanasaikolojia zinaonesha kwamba asilimia kubwa ya matatizo yanayomwangalia  binadamu yanatokana  na yeye mwenyewe  au jamaa zake, huku ushahidi  ukionesha  kuwa hata magonjwa ya kutisha kama moyo, kansa kisukari, vidonda vya tumbo na mengineyo yanachangiwa na  kiasi kikubwa na mawazo ya mtu mwenyewe.  Magonjwa mengi hayapo ila watu wanayazalisha katika nafsi zao mwishowe yanaenda kutokea kwa hofu zao na woga waliokuwa nao.

Karibu katika Blog yetu uendelee kupata mambo mengine mengi muhimu ili uweze kujikwamua na hali ya kushindwa na kuweza kushinda katika kila eneo la maisha yako na kupona magonjwa yako yanayokusumbua kwa muda mrefu.


Na: Lusako Mwakiluma Maheri

Wednesday, May 20, 2015

JINSI YA KUFANIKIWA NA KUWA TAJIRI


Jinsi ya kupata mafanikio: Ufunguo wa utajiri na kufanikiwa ebu soma haya kwa makini:
Utajiri na mafanikio sio  karama ya watu wachache. Wote tunao uwezo wa  kuupata kwa kiasi tunachotaka katika maisha yetu.  Jifunze siri ya nguvu za kupata mafanikio, utajiri kwa haraka katika maisha yako.

Kwa nini watu wengi wanataka kufanikiwa, utajiri na kwenda mbele katika maisha na wengi wetu hatuna hivyo vitu.

Kwanini?
Sababu kubwa ni kwamba tunafikiria sana hasi au tunafikiria vitu vibaya.   Kutokana na kufikiria kinyume na vibaya tunaenda kupoteza muda mwingi kwa kujiwekea vipingamizi wenyewe vya mafanikio.

Tunapoteza muda mwingi kwenye vile tunavyovikosa na kuja kuwa wafungwa  katika mafikirio yetu. Ili tuweze kupata  mafanikio katika maisha inabidi tubadilishe mtazamo wetu na tabia ambayo tumeishaizoea.

Ondoa hali ya hasi na karibisha kukua katika mafanikio yako. 
Unatakiwa uondoe kabisa hali ya hasi katika fikra zako zote na mawazo yako yote angalia mbele na jiweke vizuri katika kila unachokifanya na kwa mtu wowote unayekutana naye.  Tunajifunza kutoa shukrani kidogo  ili tuweze kuona  kile ambacho tunakosa  na kile ambacho tutakiongeza au fursa zikoje?

Unatakiwa uwe makini sana  na kila kitu kimoja, mtu au  sehemu ambayo ni muhimu katika kupata fursa  kwa hiyo utaenda kupata  kukua kimafanikio, fursa na hata  kupata utajiri unaoutaka katika maisha yako.

Usiruhusu mawazo hasi  yakuaribie mtazamo wako au nafasi ya kupata fursa, mafanikio na furaha, tengeneza tabia ya kuangalia vizuri katika kila kitu hivyo basi  usiangalie chini ambako hakuna fursa.  Kama utaona hakuna kitu, jifunze jinsi ya kuona kuwa mtazamo ni sehemu ndogo ya ukweli na upige picha kwa kupitia umuhimu na uwezekano wa kufanya kitu.

Njia za kuweza kupata  mafanikio na utajiri
·         Panga mipango: Fahamu kwamba  kama unataka kufanikiwa.  Panga mipango yako. Jiangalie mwenyewe  kama mtu  ambaye unao uwezo wa kufikia malengo yako.

·         Jiangalia tokea ndani: Fuata nafsi yako inasema nini wakati wote  kukuhakikishia msaada  kwa kuona mbele hasa wakati  ule ambao unahitaji msaada.  Nafsi ni ngumu kuelezea ila kila mmoja anajua na anao uzoefu wa mawazo makubwa kuhusiana na kitu fulani na wakati wote unaweza ukajitenga na kuumia.

·         Piga picha: Pata mafanikio na utajiri  kwa kupiga picha mipango yako na fanyia mazoezi  fahamu zako kama vile umeshapata hayo mafanikio.

·         Matendo: Usifikirie kitu utakachofanya ili uweze kufikia malengo yako ila  fanya ili ufikie malengo yako.  Kama unajua unataka kubadilisha maisha yako  na mtazamo wako, fanya hivyo.  Hata kama unaona ni ngumu kwa kutoa sababu nyingi, jipe ujasiri na endelea mbele kwa kufanya mwenyewe.

·         Jifunze kutokana na uzoefu: Jifunze kutafakari na kuangalia kwa undani maisha yako, uzoefu wako, na mahusiano yako.  Jifunze kutokana na  makosa ya awali na elewa  kwanini unabadilisha  mafikirio yako na utakubalije vikwazo  katika mafikirio na imani.   Acha hali ya hasi  na kutumia nguvu ndogo inayokuzunguka kwa sababu wakati mwingine vinakusimamisha na  kukupa mzigo mkubwa.

·         Fuata shauku yako:- Mwisho napenda nikwambie kitu muhimu sana  kwa sababu ya kufanya kile unachokipenda sana, hakuna sababu ya wewe kushindwa au kuogopa kuendelea kufanya ili ufanikiwe.

Wengi wetu wanaenda na maisha wakiwa vipofu, wamekata tamaa na hawana furaha, je unayo mawasiliano ya ndani na wewe mwenyewe na yabadilishe kuwa yenye manufaa kwa mtazamo wako na utakuwa umejihakikishia  kupata mafanikio unayoyataka katika maisha yako.

Ni juu yako kuamua sasa!!

Thursday, April 2, 2015

JINSI YA KUJITAMBUA MWENYEWE


Kama binadamu unatakiwa ujitambue  ili uweze kwenda na wakati au kufanya yale ambayo yanatakiwa  kufanyika  na yale ambayo hayatakiwi kufanyika usiyafanye.
Kuna mambo  ya msingi ya kuyafanya  ili uweze kufikiria  vizuri  wakati wote.  Na kila mtu atakayekuona  atajua huyu mtu amejitambua na amejua  umuhimu wake katika jamii inayomzunguka kwani utajikubali  wakati wote  na kuwaheshimu wengine.
Moja
Fikiri vizuri (jenga mfumo wa kufikiri vizuri); mfumo huu uwe endelevu; siyo usubiri upate tatizo ndiyo uanze kufikiri  vizuri  (usiwe kama zima moto).  Hii itakusaidia  kuanza kupanda mbegu njema kwenye mawazo yako ya kina ili maisha yako ya baadaye  yawe mazuri; yatoe mbegu nzuri/njema.

Mbili
Rudisha mawazo yako nyuma, jenga picha  yako ya utotoni.  Chagua taswira moja wakati ulipokuwa mtoto jione kimwili, kimavazi na mazingira ulipokuwa (nyumbani /shuleni au popote).  Kisha rudi kwako sasa hivi ukiwa mtu mzima; jione kama ulivyo sasa hivi ukiwa unamtazama huyo mtoto ambaye  umemjengea taswira; mtoto ambaye pia ni wewe.  Mtazame  na zungumza  naye, mwambie ulidanganywa kwamba ni mbaya; huna akili, huna thamani, huwezi, hufai nk; na wewe  uliamini kwa sababu ulikuwa mtoto.  Lakini sasa umekuwa mkubwa; fahamu ukweli halisi kwamba wewe ni mzuri, una akili unaweza na una thamani  sawa na wengine; unaweza na unafaa.  Rudia zoezi hili mara kwa mara; kila wakati hakikisha  unachagua  eneo ambalo  uliambiwa  huwezi; Futa  imani zote mbaya kwenye mawazo yako ya kina.

Tatu
Ni ile ya kufanya zoezi la kurudia rudia maneno pamoja na kujenga taswira  mfano: kila wakati  jiambie ninaweza; ninafaa; nina thamani, najiamini.  Imani ni muhimu sana wakati unajimbia maneno hayo.

Nne
Hapa utaenda kutumia mshumaa, uwashe mshumaa; uweke mbele yako juu ya meza au stuli au sehemu yoyote.  Angalia ile sehemu  ya mshumaa inayowaka moto (siyo mshumaa wote) kwa muda wa dakika 10, 30 au zaidi.  Baada ya hapo fumba macho yako yote ili uuone ule moto wa mshumaa  kwa kutumia macho yako ya akili (yaani jicho la tatu).  Utaenda kuona moto huo ukiwa wa kijani, bluu, njano au mweupe.  Baada ya kuuona, anza kuchoma zile tabia  au mambo  yanayokukera au kuwakera  wengine mfano: Choyo, wivu, uzinzi, dharau, zichome  moja baada ya nyingine.  Wakati unazichoma utaona moto wa mshumaa ukiongezeka  ukubwa au utaona moshi.  Fanya zoezi hili mara kwa mara. Baada ya muda utashangaa kuona tabia au mambo hayo yamekwisha na tabia hizo umeziacha kabisa.

Tano
Ni ile hali ya kutumia kioo, simama jitazame kwenye kioo ikiwezekana kila siku asubuhi na jioni.  Tafuta zile kasoro ambazo uliambiwa  na jiambie kwamba huna.  Kama uliambiwa wewe ni mbaya; Basi jiambie wewe ni mzuri, huku ukijiangalia bila kujiogopa kwenye kioo.  Lakini kama uliambiwa huwezi, jiambie naweza sana.  Pia jikubaai kama ulivyo na jiambie umekamilika, una thamani na unastahili.

Sita
Ni ile hali ya kupata nafasi ya kuyapa mawazo yako ya kawaida  baada ya kupewa nafasi ya muda  hatimaye yatachukuliwa mawazo yako ya kina, mambo haya  mapya  yataua au kukausha ile miche/miti iliyoota  kwenye mawazo  yako ya kina; miti hii ni ile ya mambo ambayo yanakukera au kuwakera wengine. Kwa ile ambayo imeshazaa matunda haiwezi kukauka kwani umeshaanza kuvuna kitu ambacho nidyo maisha unayoishi hivi sasa.  Njia hizo zote tano ni za mzunguko.  Hii ya sita  ni ya njia ya mkato kwani unaenda moja kwa moja  kwenye mawazo yako ya kina na kuyaambia yale unayoyahitaji ambayo ni kinyume na yanayokukera.

Nguvu ya uumbaji kitaswira  na kujipa nguvu
(i)                 Kumbuka: Imani – hisia- matokeo
(ii)               Ondoa mipango ya zamani kwenye  mawazo ya kina ndiyo sababu ya msingi ya kukwama kwani nyuma ni historia na inatia uchungu ukiifikiria.

Kuna aina tatu ya uumbaji  kitaswira: sauti, kuona na hisia.
(iv)             Kila mmoja ana aina yenye kutawala kwake awe anajua au la.  Kuna wengine  wanatawaliwa  na aina mbili.  Katika matumizi ya uumbaji kitaswira, tunaanza na aina yetu, baadaye tunajifunza nyingine.

(v)               Ili kujua aina yako, jaribu kufikiria unachohitaji sasa hivi ili uone.  Mwanzoni unaweza kusikia  sauti inayokuambia hutaweza au ni mzaha ufanyao.  Unatakiwa ufanye  mazoezi  mengi ili uweze kujenga uwezo wako ulionao au uliopotea.

(vi)             Mawazo yako ndiyo  yenye  kukufanya/kukuwezesha ujenge uumbaji kitaswira.  Unachokiona kila siku ni matokeo ya kilicho  mawazoni kila siku. Hivyo, bila kujua huwa tunaumba yale tusiyoyataka maishani.  Uumbaji  kitaswira unawakilisha utunzaji wa mbegu (mawazo) kutegemea  ni mbegu gani tumepanda.

(vii)           Makosa  yajitokeza sana; usiweke  nguvu  kwenye kukosa, kwenye usichotaka na kwenye usichonacho.   Mfano: kama umepanga kwenye chumba  kimoja na unataka kujenga nyumba yako, usijiambie nimechoka  kukaa kwenye  haka kakibanda au maisha ya kupanga yamenichosha.  Sema lazima niambie nyumbani kwangu yaani nyumba niliyojenga mwenyewe.

(viii)         Unapokuwa  kwenye uumbaji  kitaswira, hisi au  ona kama vile jambo limeshakuwa  tayari – piga picha ya utayari wa jambo lako.

(ix)                                                                                   Jinsi ya kufanya (hatua);
(i)                 Tafuta mahali tulivu
(ii)               Tuliza mawazo yako
(iii)             Weka nguvu zako  za mawazo  katika jambo  unalolitaka

(x)                Simamia kufikiria vizuri wakati wote utakaokuwanao na utashangaa kuona matokeo mazuri na kwa muda mfupi sana.

Na: Lusako Mwakiluma

Friday, January 17, 2014

HERI YA MWAKA MPYA 2014 KWA WAGENI WETU!!!!

Mkurugenzi wa WezeshaTrust Fund napenda kwatakia heri ya Mwaka mpya wenye mafanikio watembeleaji wote katika Blog yetu na Mungu awabariki sana. 

Napenda kuwafahamisha kwamba tutaanza kurusha mada mbalimbali kuhusu maisha, changamoto na mafanikio katika kila nyanja ili kuhakisha umaskini na ujinga unapungua kama sio kwisha kabisa naomba muwe tayari kupitia kila siku iitwapo leo kwenye Blog yetu kwa watanzania itakuwa ni kiswahili kwa watu wa nje watabadili lugha kama desturi yetu!!!

Bi Lusako Mwakiluma

Thursday, October 31, 2013

KONGAMANO “KIJANA JITAMBUE KUNA FURSA MBELE YAKO”


Wezesha Trust Fund & Victory Youth Support Organization kwa pamoja wamefanya kongamano la vijana waishio katika mazingira magumu Mkoani Morogoro lenye dhima "KIJANA JITAMBUE KUNA FURSA MBELE YAKO" kongamano lilifanyika katika Ukumbi wa UNGO(Umoja wa Asasi sizizo za kiserikali) Jengo la CCM Mkoa wa Morogoro.  Vijana arobaini na 48 walihudhuria na wamejifunza mambo mengi yenye maana katika maisha yao kati ya vitu walivyojifunza kwenye kongamano:-
  • Jinsi ya kijana kujitambua
  • Jinsi ya kubadilisha unavyofikiria kama kijana wa leo na kufungua macho
  •   Mikakati iliyoandaliwa kuwaletea vijana maendeleo Mkoani Morogoro
  •  Mikakati iliyowekwa na kuonyesha fursa kwa vijana kama mikopo, kuboresha elimu zao, mbinu za kuwainua kiuchumi, kuwapatia ajira wasio na ajira na fursa nyingine nyingi kutegemea na kijana yuko wapi na anataka nini kwa wakati huo.
Picha za vijana waliohudhuria pamoja na waandishi wa habari
 
Picha ya Mkurugenzi wa Wezesha Trust Fund Bi Lusako Mwakiluma akitoa mada ya elimu ya utambuzi kwa vijana wajitambue na kujua thamani yao kabla ya kupata fursa

  
Mkurugenzi wa Victory Youth Support Organisation  Bw. Freddy Ng'atigwa  akielimisha vijana fursa zilizopo na jinsi ya kuzipata