Thursday, October 31, 2013

KONGAMANO “KIJANA JITAMBUE KUNA FURSA MBELE YAKO”


Wezesha Trust Fund & Victory Youth Support Organization kwa pamoja wamefanya kongamano la vijana waishio katika mazingira magumu Mkoani Morogoro lenye dhima "KIJANA JITAMBUE KUNA FURSA MBELE YAKO" kongamano lilifanyika katika Ukumbi wa UNGO(Umoja wa Asasi sizizo za kiserikali) Jengo la CCM Mkoa wa Morogoro.  Vijana arobaini na 48 walihudhuria na wamejifunza mambo mengi yenye maana katika maisha yao kati ya vitu walivyojifunza kwenye kongamano:-
  • Jinsi ya kijana kujitambua
  • Jinsi ya kubadilisha unavyofikiria kama kijana wa leo na kufungua macho
  •   Mikakati iliyoandaliwa kuwaletea vijana maendeleo Mkoani Morogoro
  •  Mikakati iliyowekwa na kuonyesha fursa kwa vijana kama mikopo, kuboresha elimu zao, mbinu za kuwainua kiuchumi, kuwapatia ajira wasio na ajira na fursa nyingine nyingi kutegemea na kijana yuko wapi na anataka nini kwa wakati huo.
Picha za vijana waliohudhuria pamoja na waandishi wa habari
 
Picha ya Mkurugenzi wa Wezesha Trust Fund Bi Lusako Mwakiluma akitoa mada ya elimu ya utambuzi kwa vijana wajitambue na kujua thamani yao kabla ya kupata fursa

  
Mkurugenzi wa Victory Youth Support Organisation  Bw. Freddy Ng'atigwa  akielimisha vijana fursa zilizopo na jinsi ya kuzipata

No comments:

Post a Comment