Tuesday, July 7, 2015

UMUHIMU WA ELIMU YA NAFSI NA UFAHAMU


Huwezi hata kidogo kutenganisha maisha ya mwanadamu na elimu ya saikolojia, elimu ambayo katika ulimwengu wa sasa wengi wanaisikia  lakini wachache wanaotambua umuhimu wake, achilia mbali maana ya neno lenyewe.  Mimi nimeona nikupe maarifa haya baada ya kuona mwenyewe inanisaidia na pia kupitia Asasi ya WEZESHA TRUST FUND imewasaidia wengi na watu wamepona magonjwa, wameshinda majaribu na leo hii wanafurahia kuifahamu naomba na wewe uwe mmoja wao ambaye ukisoma mada hii utajua jinsi ya kuenenda.

Injinia wa  kwanza aliyeipa nguvu elimu hiii ni  mwanasaikolojia  wa Kijerumani, Wilhelm Wundt ambaye alifungua maabara  na kutibu watu kwa kisaikolojia, zoezi ambalo  lilileta matokeo  ya kushangaza ulimwengu mzima.  Huo ulikuwa ni mwaka 1879.

Saikolojia ni ‘mtoto’ wa neno la Kigiriki lijulikanalo kama ‘psyche’ au akili na roho jina ambalo baadae  lilikuzwa  na kufahamika  kama ‘Psychology’, tafsiri  ikiwa Elimu ya Nafsi  na Ufahamu.  Katika nchi zilizoendelea somo hili linapewa nafasi  ya juu katika maisha ya binadamu kutokana na  umuhimu wake.  Wanasema wataalamu kuwa, kuishi  bila kujua tabia za vitu na watu pia na  ukuaji wake na kujifunza mabadiliko yake ni sawa na kutembea katika kamba ndogo ya maisha salama.  Unatakiwa ufahamu watu, wanyama, ndege na vitu vinavyokuzunguka ili uweze kushinda majaribu au changamoto zinazokuzunguka.

Saikolojia ni somo ambalo kila kukicha binadamu anatakiwa kufundishwa kwa vile hakuna anachoweza kukifanya kisiguse  akili na  nafsi  yake.   Inashauriwa  kwamba ni lazima mtu ajifahamu  mwenyewe pia awafahamu wengine, mazingira anayoishi na mabadiliko yake wakati wote, tunaishi katika nyakati na majira na unatakiwa ufahamu kila jambo linakupata linaanzia ndani yako mwenyewe.  Unaweza ukalitengeneza bila kufahamu au mazingira yakalitengeneza ukijua kabla haikusumbui.

Maswali ya msingi yenye kumuongoza  binadamu  vizuri katika  maisha yake ni  haya.  Mimi ni nani, kwa nini niko hivi?  Wale ni  watu ni akina nani?  Kwanini wako  vile na tunapaswa  kuwa vipi baadaye, pamoja na kujiuliza kwa nini vitu vipo kama vilivyo.
Imebainika kwamba, mvutano  wa nguvu za dunia na za binadamu huongezeka mara dufu kwa mtu ambaye hajui Saikolojia ya Maisha.   Dunia kama sayari na mwanadamu kama kiumbe kila  mmoja amekuwa akitengeneza  nguvu zake za kumuwezesha  kuwepo, huku uzalishaji  wa nguvu hizo kwa upande mmoja ukikinzana vikali na mwingine, hata hivyo madhara makubwa  yamekuwa yakiwakuta  binadamu ambao ndani yao kuna uhai ambao ni sisi wenyewe.

Hata hivyo, uchunguzi  unaonyesha kwamba ufahamu, nafsi na akili umebaki kuwa kinga muhimu ya mwanadamu katika  ulimwengu huu ambao umekuwa unabadilika  mara kwa mara.  Hatari iliyokuwepo siku hizi ni  hasa kwa ulimwengu huu wa tatu ni ukosefu wa elimu hii muhimu, jambao ambalo limewafanya watu  wenyewe kwa wenyewe kuzalishiana nguvu za kuangamizana  na kuiacha dunia  ikishinda mara zote na watu kupoteza maisha pasipo muda wao kufika au kuharibikiwa na mambo yao wakidhani ni hali ya kawaida.

Inahuzunisha  pia kufahamu  kwamba mbali  na binadamu kushindana na  mabadiliko  ya ulimwengu na nguvu zake, wengi wao  wamekuwa  wakipambana  na nguvu zao wenyewe ndani ya  miili yao bila kujijua, kiasi cha kupoteza maisha.

Tafiti za wanasaikolojia zinaonesha kwamba asilimia kubwa ya matatizo yanayomwangalia  binadamu yanatokana  na yeye mwenyewe  au jamaa zake, huku ushahidi  ukionesha  kuwa hata magonjwa ya kutisha kama moyo, kansa kisukari, vidonda vya tumbo na mengineyo yanachangiwa na  kiasi kikubwa na mawazo ya mtu mwenyewe.  Magonjwa mengi hayapo ila watu wanayazalisha katika nafsi zao mwishowe yanaenda kutokea kwa hofu zao na woga waliokuwa nao.

Karibu katika Blog yetu uendelee kupata mambo mengine mengi muhimu ili uweze kujikwamua na hali ya kushindwa na kuweza kushinda katika kila eneo la maisha yako na kupona magonjwa yako yanayokusumbua kwa muda mrefu.


Na: Lusako Mwakiluma Maheri

No comments:

Post a Comment