Wednesday, May 20, 2015

JINSI YA KUFANIKIWA NA KUWA TAJIRI


Jinsi ya kupata mafanikio: Ufunguo wa utajiri na kufanikiwa ebu soma haya kwa makini:
Utajiri na mafanikio sio  karama ya watu wachache. Wote tunao uwezo wa  kuupata kwa kiasi tunachotaka katika maisha yetu.  Jifunze siri ya nguvu za kupata mafanikio, utajiri kwa haraka katika maisha yako.

Kwa nini watu wengi wanataka kufanikiwa, utajiri na kwenda mbele katika maisha na wengi wetu hatuna hivyo vitu.

Kwanini?
Sababu kubwa ni kwamba tunafikiria sana hasi au tunafikiria vitu vibaya.   Kutokana na kufikiria kinyume na vibaya tunaenda kupoteza muda mwingi kwa kujiwekea vipingamizi wenyewe vya mafanikio.

Tunapoteza muda mwingi kwenye vile tunavyovikosa na kuja kuwa wafungwa  katika mafikirio yetu. Ili tuweze kupata  mafanikio katika maisha inabidi tubadilishe mtazamo wetu na tabia ambayo tumeishaizoea.

Ondoa hali ya hasi na karibisha kukua katika mafanikio yako. 
Unatakiwa uondoe kabisa hali ya hasi katika fikra zako zote na mawazo yako yote angalia mbele na jiweke vizuri katika kila unachokifanya na kwa mtu wowote unayekutana naye.  Tunajifunza kutoa shukrani kidogo  ili tuweze kuona  kile ambacho tunakosa  na kile ambacho tutakiongeza au fursa zikoje?

Unatakiwa uwe makini sana  na kila kitu kimoja, mtu au  sehemu ambayo ni muhimu katika kupata fursa  kwa hiyo utaenda kupata  kukua kimafanikio, fursa na hata  kupata utajiri unaoutaka katika maisha yako.

Usiruhusu mawazo hasi  yakuaribie mtazamo wako au nafasi ya kupata fursa, mafanikio na furaha, tengeneza tabia ya kuangalia vizuri katika kila kitu hivyo basi  usiangalie chini ambako hakuna fursa.  Kama utaona hakuna kitu, jifunze jinsi ya kuona kuwa mtazamo ni sehemu ndogo ya ukweli na upige picha kwa kupitia umuhimu na uwezekano wa kufanya kitu.

Njia za kuweza kupata  mafanikio na utajiri
·         Panga mipango: Fahamu kwamba  kama unataka kufanikiwa.  Panga mipango yako. Jiangalie mwenyewe  kama mtu  ambaye unao uwezo wa kufikia malengo yako.

·         Jiangalia tokea ndani: Fuata nafsi yako inasema nini wakati wote  kukuhakikishia msaada  kwa kuona mbele hasa wakati  ule ambao unahitaji msaada.  Nafsi ni ngumu kuelezea ila kila mmoja anajua na anao uzoefu wa mawazo makubwa kuhusiana na kitu fulani na wakati wote unaweza ukajitenga na kuumia.

·         Piga picha: Pata mafanikio na utajiri  kwa kupiga picha mipango yako na fanyia mazoezi  fahamu zako kama vile umeshapata hayo mafanikio.

·         Matendo: Usifikirie kitu utakachofanya ili uweze kufikia malengo yako ila  fanya ili ufikie malengo yako.  Kama unajua unataka kubadilisha maisha yako  na mtazamo wako, fanya hivyo.  Hata kama unaona ni ngumu kwa kutoa sababu nyingi, jipe ujasiri na endelea mbele kwa kufanya mwenyewe.

·         Jifunze kutokana na uzoefu: Jifunze kutafakari na kuangalia kwa undani maisha yako, uzoefu wako, na mahusiano yako.  Jifunze kutokana na  makosa ya awali na elewa  kwanini unabadilisha  mafikirio yako na utakubalije vikwazo  katika mafikirio na imani.   Acha hali ya hasi  na kutumia nguvu ndogo inayokuzunguka kwa sababu wakati mwingine vinakusimamisha na  kukupa mzigo mkubwa.

·         Fuata shauku yako:- Mwisho napenda nikwambie kitu muhimu sana  kwa sababu ya kufanya kile unachokipenda sana, hakuna sababu ya wewe kushindwa au kuogopa kuendelea kufanya ili ufanikiwe.

Wengi wetu wanaenda na maisha wakiwa vipofu, wamekata tamaa na hawana furaha, je unayo mawasiliano ya ndani na wewe mwenyewe na yabadilishe kuwa yenye manufaa kwa mtazamo wako na utakuwa umejihakikishia  kupata mafanikio unayoyataka katika maisha yako.

Ni juu yako kuamua sasa!!

No comments:

Post a Comment