Wednesday, February 5, 2014

MAISHA NA ELIMU




Elimu ni ufunguo wa maisha, na elimu siku zote huwa haimtupi mtu: Kwenye Mithali 4:13 unaambiwa mkamate sana  elimu, usimwache  aende zake; mshike, maana  yeye ni uzima  wako.

Nahamasika kuwakumbusha watanzania wenzangu, maarifa ni jambo jema sana na watanzania inabidi tujifunze sana kupitia vijarida, majarida, vitabu na vitu vinatuhamasisha kujua ukweli na mambo ya dunia inavyokwenda katika ulimwengu wa leo.  Dunia inabadilika haraka sana na mimi binafsi naliona hilo naamini hata watanzania wenzangu wanaliona hilo.

 Ebu tuwekeze kwenye kujisomea vitabu mbalimbali au vijarida kama wewe ni mvivu basi soma kwa siku kurasa kadhaa zenye kukupa kitu kipya na watu wenye mambo mazuri huwa wanayaweka kwenye maandishi.  Na sio kufanya mawasiliano ya kuandikiana jumbe fupi fupi zenye kuulizana huko wapi unafanya nini, au basi turushiane mambo yenye kututoa sehemu moja kwenye nyingine.  Ebu turudi pale pale kwenye maneno ya Mungu kwani unaambiwa katika Mithali 3:20 Enenda na wenye hekima na wewe utakuwa na hekima lakini rafiki ya wapumbavu hataangamia.  Basi ebu tuchague marafiki wa kutembea nao au kufanya nao kazi, utamchaguaje mtu ambaye afikirii maendeleo yeye muda wote anataka mkae chini muanze kujadili mambo ya watu??

Ndugu, siwezi kutumia lugha ya kukulazimisha ila tushirikiane kwa pamoja kuhakikisha tunasimama katika nafasi zetu ili kuhakikisha kwamba tulipo tunahama na kuhamia mahali pa juu palipoinuka.  Kuna mtu ananiambia mimi siwezi kujiendeleza nikamuuliza kwanini, akasema nilipo hapa ofisini hata nikijiendeleza siwezi kupandishwa cheo, siwezi kupewa nafasi sahihi kwa nilichosomea nikamwambia unaujua wakati wa MUNGU? 

Basi napenda nikushirikishe elimu ni yako binafsi na mafunzo ndiyo ya kupewa na taasisi au na msaidizi wako au nduguzo.  Kwanini nimesema hayo?  Elimu inaanzia ya awali mpaka ya Chuo Kikuu na hii elimu ni kwa manufaa yako binafsi na si mtu mwingine na sio lazima elimu yako ikusaidie wewe inaweza kuwasadia watu wengine wala sio wa kwenye taasisi yako au shirika lako.  Haya basi umestaafu na wewe ni Prof.  wa Chuo ulani huo Uprofessor hauwezi kuwafundishwa wengine wa chuo kingine au jamii inayokuzunguka?  Jana wakati unasoma uliona ni ya kwako binafsi lakini leo hii unaona inavyokusaidia.

Basi tuanze sasa na tusiangalie tuna umri gani, elimu haina mwisho, na elimu ni hazina na elimu ni ufunguo wa maisha yetu ya kila siku.

Karibuni

Lusako Mwakiluma

No comments:

Post a Comment