Wednesday, April 30, 2014

“HAKUNA KUOGOPA”



Leo nataka  nikwambie kitu ambacho nimekisoma katika kitabu cha  mafanikio hayawezi kwisha na kushindwa  hakuna mwisho alisema Dr. Robert Schuller. “Usiogope  hata kama utakosea  amini katika ndoto yako.  Usihofu kama hautakwenda  kwa ajili ya ndoto  yako utakuwa  umesimama kabla Mungu hajakwambia nenda kaendelee  na kama imani yako ni ndoto basi utapata imani zaidi.


Hofu ya kufikiria kushindwa.  Hofu inayokwambia hauwezi kufanikiwa, na kama hautajaribu basi hautaweza  kupata changamoto.  Hofu wakati mwingine inaumiza.  Hofu itakusababisha usikue na kama  utasubiri kupata  maumivu ya mafanikio.

Rafiki usihofu ila  nenda na ndoto yako.  Kuna mtu mmoja zamani alisema na kijana mdogo kama utakutana na  hofu.  Usiogope ni ngumu kufikia namba mbili kama hata namba moja haujaikamilisha.  Una ndoto yako jaribu kuitendea kazi hiyo ndoto kisha utapata mambo makubwa sana. Usiogope hofu si kitu kabisa.  Ni hali inayopita tu kwani hofu ikiingia ndani yako basi jua kuna hali ya magonjwa itainuka ndani yako kama kisukari, BP na vidonda vya tumbo, maumivu ya kichwa na magonjwa mengi.

Wote tuna hofu, na tumezaliwa hivyo na sisi wenyewe ndio  tunaoweza kuhakikisha hali hii inaondoka kwa kufanya maamuzi na kuogopa hatari, ila hofu haimaanishi kwamba inaweza kutuwekea vipingamizi ili tusifanikiwe na kufanya  mambo makubwa.  Tuna maamuzi  kama tuna imani na kuamini au imani yetu au uwezekano wetu.   Kama rafiki, ndugu, mpendwa tushirikiane kuona hofu inavyofanya kazi na asiye na hofu anavyofirikia.

Hofu inaona changamoto.  Imani inaona fursa
Hofu inaona matatizo. Imani inaona jinsi ya kufikia ndoto
Hofu inaona kuna ukuta mzito. Imani inaona  kuna njia ya kutokea

Ni uamuzi wako, unaweza ukawa na imani katika hofu au  katika upande wetu.  Ebu kuwa na imani!! David Schwarz aliandika: hali ya kufikia makubwa  ni hali ya kuponya hofu kwa vitendo. Ebu elezea  hofu na kisha endelea mbele. Chukua hatua na kisha hofu yenyewe itaondoka.  Je, una imani, ebu fanya kwa vitendo na hiyo “HOFU ITAONDOKA”.

No comments:

Post a Comment