Sunday, June 8, 2014

UNAWEZA KUFANIKIWA




Hali hiyo inatakiwa uibadili kabla ya hali ya hewa haijabadilika katika maisha yako. Mawazo ya kukubali na kukataa hayatamiliki akili yako kwa wakati mmoja, lazima moja litatawala.  Wazo litakalotawala katika akili yako litatokana na uamuzi wa maisha yako, kufanikiwa au kushindwa.  Amua kufanikiwa na simama katika mafanikio.

Kumbuka njia ya mafanikio haifanywi kwa haraka, bali ni hatua kwa hatua au kidogo kidogo. Hiyo ndiyo njia ya kufanikiwa au kuwa na busara na kupata furaha katika maisha.
Ni jinsi gani kufanikiwa kuna
maana kwako. Mafanikio yana uhusiano. Ina maana kuna vitu tofauti, kwa watu tofauti. Kwa mtu binafsi inaweza kuwa rahisi kupata mafanikio kwa haraka kuliko kwa watu wengi kwa pamoja.

Kwa mwingine, anaweza kufanikiwa kuwa na nyumba nzuri na maisha mazuri ya kifamilia,Jinsi ya umuhimu wa kufanikiwa kwa mtu mmoja hakuna maana kuwa ni sawa sawa na mwingine. Kwa hali yoyote, kila mmoja anaamini kuwa mafanikio yanatokana na kutokuwa na hofu, wasiwasi, dukuduku, kukata tamaa, kushindwa na umaskini, kipato kinachompa mtu furaha, afya, amani katika akili yako, upendo, kujiheshimu, makubaliano ya kifamilia na utumiaji mzuri wa fedha.

Mafanikio huja kutokana na kutamani malengo mazuri yenye mafanikio, na kuwa mbunifu. Ina maana ili ufanikiwe katika maisha ni muhimu ukawa na malengo. Kwa nini mwingine anashindwa na mwingine anaweze kufanikiwa? Katika utafiti uliowahi kufanywa kwa nini watu wanashindwa katika maisha wakati wengine wanafanikiwa, watu mbalimbali kama wafanyabiashara, wanasaikolojia, wanafalsafa pamoja na viongozi wa dini walikuwa na maelezo tofauti.

Kutokana na utafiti huo, ilibainika kuwa, sababu ya wengine kufanikiwa na wengine kushindwa, ni kwa kuwa mtu aliyefanikiwa anajua sababu zilizomfikisha alipo pamoja na kuwa mbunifu katika kufikiri. Kwa wale walioshindwa katika maisha wamekuwa wakikabiliana na maisha pasipo na utayari wa kujua ni kwanini yupo hivyo alivyo.
Unapokuwa upande wa mafanikio, ni pale unapojua ukweli kuhusu wewe mwenyewe na kuelewa kwa nini na jinsi gani akili yako inafanya kazi na jinsi gani utafikia malengo ya maisha yako uliyojiwekea.

Mwanadamu ana mahitaji ya kiroho na kimwili pia. Kwa muonekano katika ulimwengu wa Kimagharibi, wamekuwa wakijitahidi katika jitihada za kimwili zaidi, wamekuwa wakipuuza za kiroho.  UMEZALIWA ili ufanikiwe, mtu yeyote anayekueleza tofauti na hilo, ni mjinga asiyeielewa dunia inavyokwenda na usiruhusu mtu mwingine akakusaidia kuamua jambo lako – Tulia, Tafakari kisha Chukua hatua kwa lolote linalokuhusu. Chukua akili ya kuambiwa na ya kwako changanya.

Mafanikio huwafikia wote wanaokubaliana na kanuni, pamoja na sheria zinazokuelekeza kuwa tajiri na kufanikiwa kwenye maisha.  Ujuzi huu au ukosefu wa ujuzi ni sababu ya kwanini wengine wanafanikiwa wakati wengine wanashindwa katika maisha. Kanuni hii ya jinsi gani ya mtu anaweza kufanikiwa inamfanya mtu abuni mbinu mbalimbali za kuibua vipaji vipya na kufuata sheria mbalimbali za maendeleo katika akili yake.

Mfano: unapata mshahara wa Tshs. 100,000/= inabidi huo mshahara uupange kwa jinsi ambavyo itakupelekea kuweza kuishi bila ya kumtegemea mtu mwingine kwa mahitaji yako ebu angalia mchanganuo huo hapo chini na utaona ni kwa jinsi gani unaweza kusimama na kufanikiwa katika kila jambo unalolifanya kwa kuigawanya pesa yako kwa mafungu manne na jihakikishie unaifanyia kazi hii njia bila kuwa na hofu yoyote hakika utashangaa sana utakavyoinuka kiuchumi na kufanikiwa sana:-
10% - wapatie wasiokuwa nacho; yatima, wajane, wasiojiweza
30% - Hii itakusaidia kwa kula wewe na familia yako kwa mwezi mzima
30% -Hii itakusaidia kwa ajili ya kuweka akiba na vitega uchumi
30% - Hii tumia kwa ajili ya kutumia na familia yako kwa mapumziko na furaha   ya pamoja

Sasa kama unasomesha wadogo zangu au tegemezi ebu pungu  hapo kwenye furaha pamoja na familia yako mpeleke mmoja wa tegemezi au ndugu shuleni akapate elimu ambayo itamsaidia yaani unajipunguza ili kumuongezea yeye aweze kuwa na maisha mazuri mbeleni.

Ujuzi utakapokua ndiyo silaha yako katika maisha, utakuwa tayari kuyabadili maisha yako. Kama vile mafanikio kutoka kwenye kushindwa, afya kutoka kwenye ugonjwa na furaha kutoka kwenye majonzi.  Utawala wa akili yako ni ufunguo wa mafanikio. Kile unachofikiri, kihisi na kukiamini, ndicho kitakachokuwa.  Hali ya kukata tamaa, hofu, wasiwasi na woga vinaharibu nguvu ya kujiamini na kukufanya kuwa na mawazo hasi.

Wanafalsafa wamekuwa wakifundisha kuwa, muonekano wa kimwili siyo muhimu lakini wa kiroho ni wa milele.  Mtu anaweza kimwili akawa mzuri sana lakini rohoni anakuwazia mabaya kuwa makini na marafiki, kwani kwenye biblia takatifu Mika 7:5-6 imeonyesha tuishi vipi na marafiki zetu.  Kwani adui wa kwanza ni wa nyumbani mwako.

Hivyo ni vyema mtu akajielewa mwenyewe, vitu vinavyomzunguka na watu wengine alio karibu nao.

Lusako Mwakiluma

No comments:

Post a Comment