Thursday, February 12, 2015

NJIA KUMI NA MOJA(11) ZA KUJIHAMASISHA MWENYEWE


1.      Kuwa na furaha
Amua kuwa na furaha sasa  kwa chochote  unachokifanya fanyia mchezo wa jambo hili mara zote. Fanya maamuzi  haya yatakuhamasisha wewe mwenyewe.  Jipe furaha mwenyewe shughulika na vile unavyovipenda na furaha itakuja na pia kaa na wale unaowapenda na furaha yako itakuwa ya kwako wakati wote.  

2.      Tenda kwa tabia  yako
Jinsi  unavyotenda ndivyo  utakavyokuwa mfano unatakuwa  Dr  au Prof. anza kutenda  kama Dr na Prof wanavyofanya  kazi soma sana fahamu vitu kwa kina na sio juu juu tu ingia ndani  au unataka kuwa  mwalimu fanya kama mwalimu anavyofanya  usijaribu jitahidi  ufanye kama unavyotaka bila hofu.  Itakuletea hamasa ya kuweza kuwa kama unavyotaka kwa muda mfupi sana.

3.      Kaa peke yako
Usifanye kitu, pumua na jiangalie mwenyewe kama vile mchunguzaji kwa muda kisha kwa muda utaanza  kujisikia mabadiliko mazuri yanaanza kuja kwako kwa ndani.  Mabadiliko yanaanzia ndani yako jihamasishe na utaona mabadiliko taratibu.

4.      Safisha
Safisha  mazingira yako  yanayokuzunguka kwani mazingira  ni mapana na ndiyo yanayotuvuta kwenda huku na huku na yakiwa sio masafi yatakufanya usiwe kama unavyotaka hivyo  yakiwa masafi utajisikia  vizuri mfano:Unataka kuwa mwalimu basi tengeneza  mazingira  kama walimu wanayoyatumia.

5.Tumia  kupiga picha yako
Tumia nguvu zako  kuangalia maisha yanayokuhamasisha na hamasa yako itafuata.  Mfano; unataka kujenga  nyumba piga picha ya nyumba inayoitaka halafu hii itakuletea  nawe kujihamasisha kujenga ya kwako kwa mfano ule.  Kwani picha hiyo unaweza ukaiweka katika kioo chako au chumbani mwako mahali ambapo utaenda kuiona kwa muda unaoutaka na hii itakuinua sana kuweza kupata hamasa kubwa sana.

6. Ondoa hali ya wengine wanavyokuangalia
Jipe ruhusa sasa ya kutojali watu wanasemaje kuhusu wewe.  Badala yake  weka utulivu wako na kuwafanya wengine  wajisikie vizuri wao wenyewe.   Maisha yatabadilika kama utafanya hivi wakati wote na kwa hiari yako mwenyewe bila kulazimishwa na mtu yeyote.  Unaweza kubadilisha tabia yako bila kushinikizwa na mtu yeyote katika maisha yako.  Na wale wanaokuangalia watashangaa sana kwani hawakujua kama uko kazini katika kuwafanya wajisikie vizuri wao wenyewe na kukuacha ukifanya yako bila kikwazo chochote.

7. Jiulize maswali mwenyewe 
Maswali utakayojiuliza mwenyewe yataenda kuamsha ufahamu wako:-
1.         Kitu gani kizuri kwenye maisha yako – majibu yake yatakufanya  ujue unatoka     wapi na kwenda wapi na kukitafuta hicho kizuri na kukifanyia kazi.
2.         Kitu gani  ambacho bado hakijafanyika kwako namaanisha ambacho bado haujakifanya?  - Angalia nini bado haujakifanya na kwanini haujakifanya changamoto ya kutaka kujua itakupelekea uwe jasiri wa kufanya kwa muda uliobakia hata kama muda umekwenda sana utashangaa kuona miujiza inatendeka kwa muda mfupi sana.

8. Yaangalie  tena matatizo yako
Kila suluhisho lina matatizo.  Anza kuangalia  fursa  zinazotengenezwa na matatizo yaliyopo:-
Mfano: Wauza maji walianza kuuza maji baada ya tatizo la maji kuwa kubwa katika sehemu zinazowazunguka.
Hospitali zilijengwa baada ya kuona idadi ya wagonjwa ni kubwa na hakuna mahali pa kupata matibabu wala dawa.

9. Chukua hatua za mtoto
Jaribu kuvunja vunja kile unachokitaka kwa kukipanga hatua kwa hatua.  Kisha nenda hatua moja moja kama mtoto anavyofuata hatua zake kuanzia kuzaliwa mpaka anaenda kutembea.  Hii itakusaidia sana kuweza kukamilisha mipango yako yote uliyojiwekea  na haitakuwia vigumu kuanza kwa sababu unaanza na hatua ndogo ndogo.  Utaenda kutambaa, utasimama, kisha utaanza kutembea na mwishowe kukimbia kwa hatua ndefu ndefu.

10. Pata wazo jipya
Chukua  kalamu yako na andika  malengo yako  au kitu unachotaka kufanya kwenye maisha yako.  Andika juu ya  karatasi ya kwanza na uweke orodha 1 mpaka 20.   Andika mawazo 20 kwa kujihakikishia kuyafanya. Fanya kwa kadri unavyoweza na kupenda huku ukijihamasisha mwenyewe.   Anzia namba moja mpaka ishirini kwa uhakika wa kuangalia na muda unavyokwenda ili uweze kujua ni kwa muda gani umekamilisha jambo lako ili uweze kuendelea mbele na jambo lingine.

11. Fanya kitu hata kikiwa kibaya kwanza
Usisubirie mpaka ufanye vizuri  jaribu kuanza na kukutana na changamoto ndogo na kubwa.  Cheka kwa jinsi unafurahi hata kama umekosea hali hii itakusababishia  kwenda kubadilika  nawe ndio utabadilika kwa hali unayoitaka.  Usiogope kukosea kwani wote waliokosea au kushindwa ndiyo leo hii wamefanikiwa sana.  Usiogope watu watasemaje kuhusu kushindwa kwako.  Simama katika nafasi yako na fanya kwa usahihi na Mungu atakusaidia kwani neno usiogope lina nguvu sana katika kutenda.
Na: Lusako Mwakiluma
Mhamasishaji & Mhelimishaji






No comments:

Post a Comment