Wednesday, March 25, 2015

JINSI YA KUKUTANA NA MITIHANI BILA HOFU


Hii ni hali ya kisaikolojia.  Angalia kupata zaidi kutoka na neno linalokwenda.  Uangalie  mitihani  kama mtu anayekuja kukudai deni lako na anataka wewe umlipe.   Hapo  utaongozwa na hali ya wakati huo.  Wewe ni mdeni unayedaiwa.  Wewe ni mhusika.   Kuwa mhusika mkuu au mdaiwa inakupa ujasiri.   Kuwa jasiri 

Kuwa jasiri maana yake unatakiwa kukabili hali hii bila hofu.  Mfano; Unatakiwa  sasa ulipe deni na mdeni nae  hataki kuondoka mpaka umpe pesa yake, kama ni wewe unafanyaje? Unatakiwa uwe mtulivu kisha umpe mikakati ya jinsi ya kulilipa deni aidha umechelewa  kuna sababu itabidi umpe za kumfanya aridhike na kuweza kukuongezea muda wa kuweza kulipa kama ulivyomuahidi.  Usimkimbie  wala usikatae  kuongea naye  utapoteza ujasiri wa kukabiliana na mitihani yako.

Muhammad Ali, alikuwa bingwa wa mchezo wa saikolojia.  Aliingiza hofu ndani ya moyo wake kabla ya kupigana kwa njia ya kutengeneza ushindi kabla ya pambano.   Ali alikuwa  anatafakari  ushindi wakati wote.  Alikuwa  anapigana  kisaikolojia  na mwishoni aliingia ndani ya uwanja kama mshindi siku ya pambano kwani aliweza kumsoma  anayepambana  naye kupitia  michezo ya nyuma.

Wengi wameshindwa  kumpiga Muhammad Ali na walikuwa wanapigwa kabla hata mchezo haujaanza.

Geogre Foreman alikuwa na uzito mkubwa katika siku zake za mapigano.  Watu wachache waliweza kupigwa kwenye mzunguko wa  kwanza tu walipopigana nae.  Foreman alikuwa na uzito mkubwa sana kuliko mahasimu wake.  Kabla ya mchezo ambao sitausahau na George Foreman kule Zaire.  Ali alizungumza  na dunia jinsi alivyojiandaa kupigana na huyo hasimu wake.  Alijihakikishia ushindi na alikubali  yote kwamba anaenda kufanya kitu cha tofauti.

Ndiyo, unaweza kufikiria kitu gani kilitokea  siku hiyo ya mpambano.  Kwa wakati  ule kengele  ilipopigwa kwa mara ya kwanza, George  Foreman  alikuwa ni mtu aliyepigwa tayari.  Ali alijitahidi kumtoa nje kwa mazungoko wa kwanza tu.

Jiandae na wewe kwa mtihani kama Ali alivyojiandaa kupigana na  George Foreman  na hakuwa na hofu ya kupigana naye (Work Hard, Work Smart then Trust God).

Nawasilisha.
Lusako Mwakiluma


No comments:

Post a Comment